“OZIL” AWEKA WAZI SABABU YA KUKAATA KUPUNGUZIWA MSHAHARA

12,310

Kiungo wa arsenal mesut Ozil amezungumza kwa mara ya kwanza sababu zilizo peleka yeye kukata kupunguziwa mshahara wake wakati ambapo arsenal ilitoa agizo hilo kwa wachezaji wake.

Itakumbukwa kuwa mwezi April wachezaji pamoja na wafanyikazi wote wa Arsenal walitakiwakukubali mkato huo wakati ambapo maambukizi ya corona yalikuwa yameongezeka duniani na kauthiri biashara.

Ozil amedai kuwa alikataa agizo hilo kwani usimamizi wa club haukuwa umetoa maelezo zaidi kuhsu mkato huo mabao anadai ulifanywa kwa haraka

 Vile vile amedai kuwa majukumu ya familia yake na mashirika ambayo imakuwa ikipokea msaada wake pia yalichagia yeye kudinda ombi hilo la Arsenal.

“kila mtu ana haki ya kujua kinachoendela…kwa wachezaji wachaga haikuwa sawa mimi wakati huo nilikua na mtoto mchanga familia nchiniUjuerumani na Uturuki pamoja na wakfu ambazo zinanitegemea” jarida la goal limenikuu kauli yake Ozil

 Aidha amedai kuwa kwa kipindi cha miaka miwili kumekwepo na njama ya kujaribu mkuchafulia jina kwa umma.

Ria huyu wa ujerumani ameongeza kuwa hana uhakika ikiwa uamuzi huo ndio unafanya anaachwa nje ya kikosi cha arsenal kwa sasa.

Leave A Reply

Your email address will not be published.