Mashaabiki washtushwa na taarifa ya Aubemeyang Kujiunga na Chelsea

11,295
Kwibuka30

Mshambuliaji wa klabu ya Arsenal, Pierre-Emerick Aubameyang ameshangaza watu baada ya kuibuka kwa taarifa za kuwa anafikiria kuhamia Chelsea mwezi Januari.

Aubameyang mwenye umri wa miaka 31, ameonyesha nia hiyo ya kuhamia The Blues siku moja kabla ya mchezo wao wa Fainali kombe la FA Cup.

Kwibuka30

Hata hivyo hadhima yake ya kuhamia Chelsea imeonekana kugonga mwamba baada ya Chelsea kutokuwa na kiasi kikubwa cha fedha cha kumlipa Aubameyang.

Mkataba wake unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu ujao, Aubamayeng amesajiliwa Arsenal akitokea Borussia Dortmund kwa dau la paundi milioni 56 mwaka 2018.

Kocha wa Chelsea, Frank Lampard kwa sasa anatafuta mchezaji wa safu ya ushambuliaji lakini hana msuli wa kumlipa nyota huyo raia wa Gabon na kama atahitaji kuitumia The Blues lazima Aubamayeng ashushe dau lake la mshahara.

Aubameyang amefunga jumla ya magoli 27 msimu huku Kocha wa Arsenal, Mikel Arteta akifanya kila jitihada kuhakikisha anambakiza nyota huyo ambaye pia anawindwa na Barcelona na AC Milan.

Leave A Reply

Your email address will not be published.